- Honesty

Uaminifu

Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake; - Wakolosai 3:9

Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote. - Romans 12:17

tukitangulia kufikiri yaliyo mema, si mbele za Bwana tu, ila na mbele ya wanadamu. - 2 Wakorintho 8:21

1 Mizani ya hadaa ni chukizo kwa Bwana; Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza. - Mithali
3 Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza Bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza. 11:1, 3

13 Mwenye kitango akisingizia hufunua siri; Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.
17 Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake; Aliye mkali hujisumbua mwili wake. Mithali 12:13, 17

Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema. - Mithali 28:13

Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki - Yakobo 5:16

akini tumekataa mambo ya aibu yaliyositirika, wala hatuenendi kwa hila, wala kulichanganya neno la Mungu na uongo; bali kwa kuidhihirisha iliyo kweli twajionyesha kuwa na haki, dhamiri za watu zikitushuhudia mbele za Mungu. - 2 Wakorintho 4:2